>>MGAMBO, POLISI, TOTO, 2 ZIPI KUIFUATA LYON CHINI??
DABI_YA_KARIAKOOVPL, LIGI KUU VODACOM, inafika tamati Jumamosi Mei 18 wakati tayari Bingwa ni Yanga, Mshindi wa Pili ni Azam FC na kilichobaki ni Timu zipi mbili zitaungana na African Lyon kucheza FDL Msimu ujao lakini bado BIGI MECHI ni ile ile DABI ya KARIAKOO kati ya Yanga na Simba.
Siku zote ni Bigi Mechi Yanga na Simba lakini safari hii  ‘kachumbari’ hamna maana tayari Yanga ni Bingwa na Nafasi ya Pili imechukuliwa na Azam FC na Simba watabaki Nafasi ya Tatu tu, na hivyo kutocheza Klabu Afrika Msimu ujao, lakini Siku zote Mechi hii ni ya ushindani uliojaa kila majigambo, sifa na hekaheka kila Kona ya Dar es Salaam na Nchi nzima.
Hii ndio DABI ya KARIAKOO, Mechi tangu zama za zamani ina vituko, shamrashamra na kila aina ya vioja.
Na ndio maana Timu zote, Yanga na Simba, zilipiga Kambi nje ya Dar es Salaam huko Visiwani Unguja, kwa Yanga, chini ya Kocha wao toka Uholanzi Ernie Brandts, kuwa Pemba, na Simba, chini ya Mfaransa, Patrick Liewig, kutua huko Zanzibar.
Hii ni mara ya Pili Timu hizi kukutana Msimu huu kweye VPL na mara ya kwanza matokeo yalikuwa Bao 1-1 hapo Oktoba 3, 2012.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KUMBUKUMBU TU-3 OKTOBA 2012:
YANGA 1 SIMBA 1
Simba ndio walitangulia kupata bao Dakika ya 4 tu ya mchezo kwa bao la Amri Kiemba baada ya kupokea pande zuri toka kwa Mwinyi Kazimoto.
Hadi mapumziko Simba walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Yanga walisawazisha bao kwa Penati katika Dakika ya 66 baada ya Ngalema kuunawa mpira na Penati hiyo kufungwa na Saidi Bahanuzi.
Baada ya hapo Yanga walipata pigo baada ya Chipukizi wao Simon Msuva kupewa Kadi Nyekundu kwa kumpiga Juma Nyosso.
Matokeo haya yameifanya Simba iwe na Pointi 13 kwa Mechi 5 na Yanga kuwa na Pointi 8 kwa idadi hiyo hiyo ya Mechi.
VIKOSI:
SIMBA: Juma Kaseja, Nassor Chollo, Paul Ngalema, Juma Nyosso, Shomary Kapombe, Amri Kiemba, Edward Christopher, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Haruna Moshi na Mrisho Ngassa.
Akiba: Wilbert Mweta, Komabil Keta, Paschal Ochieng, Kiggi Makassy, Salum Kinje, Daniel Akuffo, Abdallah Juma na Ramadhan Chombo ‘Redondo’
YANGA: Yaw Berko, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Cannavaro, Kevin Yondan, Athumani Iddi, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbangu, Said Bahanuzi na Hamisi Kiiza.
Akiba: Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma Abdul, Godfrey Taita, Stafano Mwasyika, Job Ibrahim, Frank Domayo, Nizar Khalfan, Shamte Ally, Idrisa Rajab na Jerry Tegete.
Refa: Mathew Akrama
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi Mei 18
Toto Africans Vs Ruvu Shooting
Mgambo JKT Vs African Lyon
JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
TZ Prisons Vs Kagera Sugar
Simba SC Vs Yanga SC
JKT Oljoro Vs Azam FC
Polisi Moro Vs Coastal Union
MSIMAMO:
***YANGA+++BINGWA
NA
TIMU
P
W
D
L
GF
GA
GD
PTS
1
YANGA
25
17
6
2
45
14
31
57
2
AZAM FC
25
15
6
4
45
20
25
51
3
SIMBA SC
25
12
9
4
38
23
15
45
4
KAGERA SUGAR
25
11
8
6
26
19
7
41
5
MTIBWA SUGAR
25
10
9
6
29
24
5
39
6
COASTAL UNION
25
8
11
6
25
23
2
35
7
RUVU SHOOTING
25
8
8
9
22
24
-2
32
8
JKT OLJORO
25
7
8
10
21
26
-5
29
9
TANZANIA PRISONS
25
7
8
10
16
22
-6
29
10
JKT RUVU
25
7
5
13
21
38
-17
26
11
MGAMBO SHOOTING
25
7
4
14
16
27
-11
25
12
POLISI MOROGORO
25
4
10
11
13
23
-10
22
13
TOTO AFRICAN
25
4
10
11
21
33
-12
22
14
AFRICAN LYON
25
5
4
16
16
38
-22
19
***AFRICAN LYON IMESHUKA DARAJA
WAOWAHI KUWA MABINGWA:
1965 Sunderland (Sasa inaitwa Simba SC)
1966 Sunderland
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans
2006 Young Africans
2007 Simba SC
2007/08 Young Africans
2008/09 Young Africans
2009/2010 Simba SC
2010/2011 Young Africans
2011/2012 Simba SC
2012/2013 Young Africans

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top