Aibu! Mrembo anayeuza nyago (video queen) kwenye video kibao za wasanii wa Bongo Fleva, Tunda Sabasitana na mchekeshaji maarufu Bongo, Stan Bakora wamepiga picha za ngono kisha kusambaa hadi kulifikia deski la Ijumaa Wikienda.

Mrembo anayeuza nyago (video queen) kwenye video kibao za wasanii wa Bongo Fleva, Tunda Sabasitana na mchekeshaji maarufu Bongo, Stan Bakora wakijiachia.
Picha hizo chafu zilitua mezani kwetu wikiendi iliyopita ikiwa ni siku mahususi kwa wapendanao.
Picha hizo zinawaonesha wawili hao wakiwa kwenye ‘bedi’ huku wakifanya yao.
Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa Stan na Tunda, wawili hao wemekuwa kwenye ‘malovee’ siku nyingi na kupiga picha za ngono kwao si ishu maana wote hawana mshipa wa aibu kwa kuwa ni wasanii.
Ilisemekana kwamba tangu Stan aanze kuigiza amekuwa akifanya mambo ya aibu tofauti na jinsi anavyoonekana.
Stan Bakora na mrembo huyo wakiendelea kula ujana.
Pia ilidaiwa kwamba Tunda naye si mwoga kwenye mambo hayo ndiyo maana hata anapoombwa kuwa katika video za wasanii mbalimbali huwa haoni aibu kujiachia mtupu.

“Tunda ni video queen ambaye ameonekana kwenye video nyingi sana za wasanii kama kwenye Wimbo wa Barnaba na Amini unaokwenda kwa jina la Why Me, wimbo wa Matonya aliomshirikisha Christian Bella wa Agwelina, wa TID mpya unaoitwa Wewe Ndo Unanipa Raha, wa Christian Bella, Dully Sykes na Tanzanite unaitwa Ndombolo ya Solo na Wimbo wa Timbulo unaoitwa Sina Makosa,” kilisema Chanzo chetu.
Wawili hao wakitomasana.
Kwa upande wake, Stan anafanya poa kwa sasa katika filamu za kuchekesha akiwa karibu na mkuu wake wa kazi, Mussa Yusuph ‘Kitale’ na wanafanya safi pia kwenye vibwagizo ambavyo vinarushwa kila mara katika Kituo cha Redio EFM.
Wawili hao walipopigiwa simu kwa nyakati tofauti hawakuwa na majibu ya kueleweka zaidi ya kujing’atang’ata kwa aibu.

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top