
Vikao hivyo vikuu vya CCM katika ngazi za mbali na kujadili
mchakato wa bunge maalum la katiba pia vimezungumzia mustakabali wa
chama hicho katika chaguzi zijazo za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu
huku katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho Nape Nauye akisema
wataendelea kujadili katiba kwani ajenda za TCD sio ajenda za CCM kwa
kuwa vikao vyake vinajitegemea na viko huru.
Akizungumzia msimao wa chama hicho kuhusu kura za maoni ya wananchi
Nape amesema CCM itaendelea kuheshimu sheria ya mabadiliko ya katiba ya
mwaka 2012 sura ya 83 inayoelekeza kura za maoni zipigwe ndani ya siku
84 baada ya bunge maalum kuvunjwa lakini pia akisisitiza sheria hiyo
inaweza kufanyiwa mabadiliko na bunge la jamuhuri ya muungano wa
Tanzania.
Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.