Friday, October 17, 2014

KAULI YA MSANII FID Q KUHUSU UMRI WA MISS TANZANIA 2014 HII HAPA


Kama ulifatilia shindano la Miss Tanzania 2014 weekend iliyopita utakua unajua kilichotokea na kinachoongelewa ikiwa ni baada ya baadhi ya watu kupinga au kutoridhishwa na matokeo ya mshindi aliyetangazwa ambae ni Sitti Mtemvu mtoto wa mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu. 
Kumekuwepo na malalamiko mengi sana hasa kwenye mitandao ya kijamii ambako zimesambazwa hadi picha zake pamoja na hati za kusafiria, ishu nyingine ikizungumzwa kwamba kuna uwezekano amedanganya umri na elimu yake.

haya ndio aliyoyaandika rapper Fid Q kuhusu malalamiko ya Watanzania yanayoendelea juu ya umri wa mrembo huyu.

Fid Q 1

Fid Q 2

SAKATA LA MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI ALIYEOLEWA, MENGINE YAIBUKA

Ilikuwa Oktoba 7 mwaka huu, saa 1.00 asubuhi katika eneo la Mbondole, Kata ya Msongola, Wilaya la Ilala mkoani Dar es Salaam kulipozuka tafrani baada ya mwanamume mmoja kukamatwa akituhumiwa kumweka kinyumba binti mwenye umri wa miaka 15.
Mama wa binti aliyewekwa kinyumba, Amina Juma anasema mshtuko alioupata baada ya kumwona binti yake akichomoza katika chumba cha mwanamume huyo, ulisababisha tumbo lake kumkata kwa uchungu.
“Sikuamini macho yangu kumuona mwanangu akitolewa katika chumba hicho, nilitamani iwe ndoto... lakini ilikuwa kweli na tukio hilo liliniumiza sana,” anasema mwanamke huyo.
Akisimulia huku machozi yakimtoka, anasema siku hiyo alipata taarifa kutoka kwa mdogo wake kuwa mwanaye anaishi na mwanamume huyo huku akifungiwa na kufuli ndani kwa kuhofia isijulikane.
Baada ya kupata taarifa hizo, walishirikiana na mdogo wake kwenda kutoa taarifa katika ofisi ya Serikali za Mtaa huo, ili waweze kumdhibiti mtuhumiwa na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. Katika ofisi hiyo, walisaidiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi ya mtaa huo, ambao walikaa kuanzia saa moja asubuhi hadi saa 8:30 mchana ili kuhakikisha mtuhumiwa huyo anakamatwa.
Mkasa ulivyoanza
Ilikuwa Agosti mwaka huu mama huyo akiwa nyumbani kwake alifika kijana mmoja ambaye alijitambulisha kuwa ni mshenga anayetaka kutoa posa kwa mwanaye. Hata hivyo, alimkatalia na kumweleza kuwa mtoto wake bado anasoma.
“Baada ya kumkatalia mshenga huyo akaanza kutumia mwanya wa kuja gengeni kwangu, ili amrubuni akubali kuolewa na huyo mwanamume lakini alikuwa anakataa,”anaelezea mama wa mtoto huyo.
Anasema siku moja mtuhumiwa alifika nyumbani kwake na kumweleza kuwa atahakikisha mwanafunzi huyo anafutwa shule, kwa kuwa amekwamisha mpango wake.
“Siku hiyo mtuhumiwa aliniongelea maneno ya ovyo, nilikasirika na kuamua kuingia ndani kulala... nilipoamka sikumkuta binti yangu.
“Nilijaribu kuwauliza majirani kama wamemwona, lakini sikupata jibu hivyo nililazimika kwenda kwa mtuhumiwa ili kumwangalia,” anasema.
Alipofika eneo hilo alimkuta kijana mmoja na kumuuliza kama mwanaye ameonekana lakini alimjibu hakumwona, wakati huo aliiona baiskeli ya mtuhumiwa huyo akiwa nje ikiashiria kuwa alikuwa ndani.
Anasema wakati alipokuwa anamwuliza kijana huyo, mara mtuhumiwa alitoka nje na baadaye alifuatia mwanaye.
Anasema kitendo hicho kilimuudhi na alimua kumwadhibu kwa kumchapa fimbo ndipo mtoto huyo alipotoroka na kwenda kwa baba yake mzazi ambaye anaishi Kivule, Wilaya ya Ilala.
Anasema siku ya pili alilazimika kwenda kumfuata ili wafanye kikao cha ndugu kuhusiana na suala hilo.
Baada ya kikao mtoto huyo alipoulizwa, alidai kuwa hataki tena shule.. “hivyo nilimchukua na kwenda naye nyumbani, lakini mume wangu wa sasa (baba mlezi wa binti huyo) alimkataa kutokana na tabia zake.”
Siku iliyofuata alilazimika kumrudisha kwa baba yake mzazi na kuwa tangu hapo hakujua tena taarifa zake mpaka lilipotokea hili.
“Mimi naona huu ulikuwa ni mchezo uliopangwa na mtuhumiwa na baba mzazi wa mtoto huyu, inaonekana alikuwa anajua mchezo mzima. Kama mwanaye hakuwapo nyumbani kwa nini hakutoa taarifa polisi? Au kwa ndugu?” anahoji.
Sakata latinga polisi
“Oktoba 10 mwaka huu nikiwa nyumbani kwangu, walikuja askari kutoka Kituo cha Polisi Stakishari, Ukonga walichukua maelezo yangu na ya mtoto na baada ya hapo waliniambia niende polisi baada ya siku tatu,” anasema.
Baada ya kutoa maelezo polisi ilifunguliwa jalada la kesi ya ubakaji lenye namba STK/RB/13749/14 na wakati huo nilipewa fomu ya polisi kwa ajili ya kwenda Hospitali ya Amana ili vichukuliwe vipimo vyote.
“Hivi unavyoniona nampeleka mwanangu katika Hospitali ya Amana ili akapime vipimo vyote ambavyo vinahitajika,” anaeleza.
Alivyomlea mwanaye
Mama huyo anasema aliachana na mumewe wa kwanza wakati binti huyo akiwa na umri wa miaka miwili na kwamba tangu wakati huo, alimlea peke yake kwa hali na mali.
Anasema alipofikisha umri wa miaka saba, alianza darasa la kwanza na hapo akaanza kumtembelea baba yake na hata kulala lakini hakuwahi kupewa fedha kwa ajili ya shule.
Binti anena
Binti huyo anasema alikutana na mwanamume huyo alipokuwa anakwenda kununua mkaa katika banda lake lililopo katika eneo hilo la Kigezi.
Anasema mwanamume huyo alikuwa akimlaghai kwa kumwambia kuwa ameshakuwa mtu mzima hivyo aache shule aolewe.
Akiwa kwa baba yake mzazi, binti huyo anasema mwanamume huyo alikuwa akivizia baba huyo anapoondoka naye anamfuata na kumweleza kuwa anataka kumpeleka mshenga, lakini baadaye alimtorosha.
“Nilianza kuishi naye mwezi uliopita, alinitorosha kutoka Kivule kwa baba yangu mzazi na kunipeleka nyumbani kwake Mbondole,” anasimulia.
Anasema wakati huo alimweleza kuwa ana watoto watatu wanaotakiwa kulelewa kwa kuwa aliachana na mama yao.
Mwanamume aliyekuwa anaishi naye alikuwa anafanya biashara ya kuuza mkaa eneo la Kigezi na kila siku alikuwa akimwachia Sh5,000 kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Viongozi wa Serikali wafunguka
Mjumbe wa Kamati ya Ulinzi wa Mtaa huo, Julius Meng’anya anasema baada ya kupewa taarifa hizo walikwenda hadi kwenye nyumba hiyo ili kumkamata mtuhumiwa. Walifika asubuhi eneo kwa ajili ya kulinda na kuhakikisha mtuhumiwa huyo wanamdhibiti na ilipofika saa 8.30 mchana aliporudi nyumbani kwake walimkamata pamoja na mwanafunzi huyo.
Baada ya kumkamata walimtaarifu mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo ambaye alifika kwenye eneo hilo lakini cha kushangaza alimwachia huru mtuhumiwa huyo.
“Kwa kweli kitendo cha mwenyekiti kumwachia mtuhumiwa huyo kilituudhi sana tulitegemea mtuhumiwa angechukuliwa hatua za kisheria,” anasema Meng’anya.
Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa huo, Salum Matangula alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa alikiri mbele ya kikao kuwa alipewa ruhusa na mama mzazi wa mtoto huyo ili aishi naye.
Anasema kutokana na maelezo ya pande zote, walibaini kuwa wote wana makosa ndipo walipomtaka mama huyo aende kwenye duka la dawa ili achukuliwe kipimo cha mimba na baada ya hapo ampeleke mwanafunzi huyo shuleni.
“Niliwaeleza kuwa wote wana makosa, mama alikuwa anadai mwanaye akapime kwanza, nikamruhusu, lakini sijapata majibu hadi leo,” anasema Matangula.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kigezi anayosoma mtoto huyo, Joseph Kalungutu anasema mwanafunzi huyo ni mtoro na kipindi cha nyuma alikuwa akihudhuria darasani mara moja moja na lakini kuanzia Septemba, mwaka huu, hakuonekana kabisa shuleni.
“Mahudhurio yake ni mabaya, baada ya kuona maudhurio yake siyo mazuri nilimwita mama yake ambaye alidai kuwa hayupo anaishi kwa baba yake mzazi,” anasema Kalungutu.
Anasema Septemba mwaka huu akiwa shuleni hapo alikwenda mwanamume aliyejitambulisha kuwa mzazi wa binti huyo akidai kuwa amekwenda hapo kwa ajili ya kumfuta shule mwanaye kwa kuwa anaonekana mkubwa.
“Nilimkatalia na kumweleza kuwa sheria hairuhusu mwanafunzi yeyote aliyeandikishwa kufutwa shule hadi hapo atakapomaliza. Nilimweleza kuwa yeyote anayejaribu kufanya hivyo lazima afikishwe kwenye vyombo vya sheria.
Mwanamume anayedaiwa kumtorosha binti huyo, Halifa Ally anakiri kuwa aliishi naye... “Sina cha kukueleza zaidi ya hayo ninachofahamu huyo binti nilikuwa naishi naye,” anasema Ally.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki anasema Ally anayetuhumiwa kuishi na binti huyo ametoroka... “lakini polisi inawahoji mama wa mtoto huyo pamoja na mwanaye katika Kituo cha Polisi cha Stakishari huku tukiendelea kumtafuta mtuhumiwa ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria,” anasema Nzuki.

CCM YADAI MAKUBALIANO YA RAIS NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA HAYAZUII MCHAKATO WA KATIBA MPYA KUENDELEA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhpo9BYTJkvFT-eLQNTFZTJHcQ6xfkPAbdvjQIy4GUKIb4KuWs0Ix28vIX9QWHl725ky632bSUpugVXSYbb90oenj2JK2_4SrMWQ0OYa8a40VeKX6PlU1NlhOvjysC-FUfjKVvaxyC3Fho/s1600/MMGM4299.jpgKamati kuu na halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi {NEC} zimekutana mjini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine vikao hivyo vimejadili mchakato wa bunge la katiba na kubainisha mafanikiano ya upatikanaji wa katiba mpya kati ya Rais Jakaya Kikwete na vyama vya siasa vinavyiunda kituo cha Demokrasia Tanzania {TCD} hayazuii chama hicho kuendelea na mchakato wa katiba.
 
Vikao hivyo vikuu vya CCM katika ngazi za mbali na kujadili mchakato wa bunge maalum la katiba pia vimezungumzia mustakabali wa chama hicho katika chaguzi zijazo za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu huku katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho Nape Nauye akisema wataendelea kujadili katiba kwani ajenda za TCD sio ajenda za CCM kwa kuwa vikao vyake vinajitegemea na viko huru.
 
Akizungumzia msimao wa chama hicho kuhusu kura za maoni ya wananchi Nape amesema CCM itaendelea kuheshimu sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012 sura ya 83 inayoelekeza kura za maoni zipigwe ndani ya siku 84 baada ya bunge maalum kuvunjwa lakini pia akisisitiza sheria hiyo inaweza kufanyiwa mabadiliko na bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania.

CCM YADAI MAKUBALIANO YA RAIS NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA HAYAZUII MCHAKATO WA KATIBA MPYA KUENDELEA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhpo9BYTJkvFT-eLQNTFZTJHcQ6xfkPAbdvjQIy4GUKIb4KuWs0Ix28vIX9QWHl725ky632bSUpugVXSYbb90oenj2JK2_4SrMWQ0OYa8a40VeKX6PlU1NlhOvjysC-FUfjKVvaxyC3Fho/s1600/MMGM4299.jpgKamati kuu na halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi {NEC} zimekutana mjini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine vikao hivyo vimejadili mchakato wa bunge la katiba na kubainisha mafanikiano ya upatikanaji wa katiba mpya kati ya Rais Jakaya Kikwete na vyama vya siasa vinavyiunda kituo cha Demokrasia Tanzania {TCD} hayazuii chama hicho kuendelea na mchakato wa katiba.
 
Vikao hivyo vikuu vya CCM katika ngazi za mbali na kujadili mchakato wa bunge maalum la katiba pia vimezungumzia mustakabali wa chama hicho katika chaguzi zijazo za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu huku katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho Nape Nauye akisema wataendelea kujadili katiba kwani ajenda za TCD sio ajenda za CCM kwa kuwa vikao vyake vinajitegemea na viko huru.
 
Akizungumzia msimao wa chama hicho kuhusu kura za maoni ya wananchi Nape amesema CCM itaendelea kuheshimu sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012 sura ya 83 inayoelekeza kura za maoni zipigwe ndani ya siku 84 baada ya bunge maalum kuvunjwa lakini pia akisisitiza sheria hiyo inaweza kufanyiwa mabadiliko na bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania.

USHIRIKINA WASABABISHA WANAWAKE WAWILI WA FAMILIA MOJA KUCHINJWA HUKO SHINYANGA



Wanawake wawili kutoka familia moja wakazi wa kitongoji cha Nanzilo kijiji cha Ihugi,kata ya Lyamidati tarafa ya Nindo wilaya ya Shinyanga vijijini wameuawa kikatili baada ya kuchinjwa kwa panga na watu wasiofahamika wakati wakijiandaa kula chakula cha usiku.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga SACP Justus Kamugisha amesema tukio hilo limetokea Oktoba 14 mwaka huu saa mbili usiku na kuwataja wanawake waliouawa kuwa ni Dilu Tungu(80) na mtoto wake Bunya Mihangwa(45).

Kamanda Kamugisha amesema wanawake hao wakiwa wakijiandaa kula chakula cha usiku na wanafamilia wenzao  ghafla walivamiwa na watu watatu wasiofahamika kisha kuanza kuwakata kwa panga sehemu mbalimbali za miili yao kisha kuwachinja shingo hadi wakapoteza maisha.

Chanzo cha tukio hilo kinatajwa kuwa ni imani za kishirikina kwani kuna mwanamme aitwaye Bwanya Mlyashimba(40) (ambaye anashikiliwa na polisi) mkazi wa Ihugi alikuwa akiwatuhumu marehemu hao kwamba walimroga yeye na kusababisha akose nguvu za kiume na kwamba walimroga 
 mama yake Hollo Mahangwa aliyefariki dunia mwaka 2013.
Tayari Bwanya Mlyashimba anashikiliwa na jeshi la polisi watuhumiwa wengine wanasakwa.

MAMA ANYWESHWA JUISI KISHA KUIBIWA MTOTO WA SIKU 4


Mtoto mwenye umri wa siku nane, ameibwa baada ya mama yake kunyweshwa juisi inayosadikiwa kuwa na dawa za kulevya.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma, Dk. Nassoro Mzee, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mwanamke huyo, Teddy Bishaliza (19), alilazwa katika Wodi 17 kufuatia afya yake kuathiriwa na dawa hizo, huku mtoto wake wa kike ikidaiwa kuwa aliibwa katika tukio lililotokea juzi mtaa wa Chidachi, Manispaa ya Dodoma.

Akizungumza kwa tabu wodini hapo, Bishaliza alisema alijifungua mtoto huyo Jumatano ya wiki iliyopita hospitalini hapo kwenye Wodi Namba Tatu na kuruhusiwa kurejea nyumbani na mtoto wake siku iliyofuata.

“Nikitoka wodini, nilikutana na dada ambaye sikuwahi kumuona, akanisaidia kubeba mizigo michache niliyokuwa nayo na tulipokaa kwenye benchi akaniambia anikodie bajaj inipeleke nyumbani, tulipofika hakuteremka kwenye bajaj akaahidi kuja tena kututembelea,” alisimulia Bishaliza.

Alisema juzi jioni, dada huyo alifika nyumbani kwao akiwa amevaa dera na kujitanda kikoi kizito chenye rangi ya kijani na chungwa bivu, baadaye mama yake Bishaliza, alimpelekea chakula kisha akamuacha na mdogo wake, Rahel Leganga (12), mtoto na mgeni wao huyo.

Rahel alilieleza  kwamba wakati wakila chakula, mgeni ambaye baada ya mama Teddy kuondoka alijifungua ushungi aliokuwa amejifunika sehemu kubwa ya uso wake na kumwagiza  ampe vikombe ili awawekee juisi.

“Alitoa juisi ya boksi ile inayouzwa Shilingi 3,000, akanimiminia dada kikombe cha nusu lita na mimi akaniwekea, nilipoonja nikahisi chungu nikaikataa, lakini dada akanywa yote,” alisimulia Rahel na kuendelea:

“Akaniambia ninywe ili niongeze damu mwilini, nikitaka nisisikie uchungu ninywe haraka haraka kama maji, nikamwambia mimi siinywi, tulipomaliza kula tu dada akasema anahisi usingizi, akalala.”

Rahel alisema hata yeye baada ya kula na kurejesha vyombo mahala pake, alilala na alipoamka saa 11:00 alfajiri ya jana, alishangaa kumkuta dada yake amelala fofofo huku mtoto na mgeni wakiwa hawamo chumbani.

Alisema baada ya dada yake kuamka, walijaribu kutoka nje, lakini ilibainika mlango ulifungwa kwa nje, majirani walisaidia kuufungua baada ya wao kupiga kelele wakiomba msaada, yeye (Rahel) alikwenda kumuita baba na mama yao wanaoishi mtaa wa pili.

Baba na Mama Teddy wakiwa nje ya wodi namba 17 alimolazwa mtoto wao huyo, walisema kati yao hakuna anayeweza kumtambua mwizi wa mjukuu wao, isipokuwa Rahel aliyesema akimuona mwanamke huyo atambua.

Baba Teddy aliyejitambulisha kwa jina la Job Leganga, alieleza
kuwa Teddy hana mume bali alipata ujauzito na kutokana na nyumba yao kuwa ndogo, waliamua kumpangishia chumba mtaa wa pili kutoka nyumbani kwao ili waendelee kumhudumia kwa mahitaji yake muhimu.

Teddy alitaja jina la baba wa mtoto wake kuwa ni Christian Francis, ambaye hata hivyo, aliondoka mjini hapa na kurejea kwao mkoani Morogoro.

MAJIRANI WASIMULIA
John Nadoo (50), Mjumbe wa Nyumba Kumi katika eneo analoishi Teddy, alisema juzi jioni alimuona mwanamke akiwa amevaa dera, amejitanda mtandio wake kiasi cha kubakiza sehemu ndogo ya sura yake, lakini hakumsalimia badala yake alionekana akiita watoto.

“Baada ya kuzungumza na watoto, niliona akiongozana na mtoto mmoja, sikuelewa kilichoendelea mpaka asubuhi nilipopata taarifa kutoka kwa majirani kuwa mtoto wa Teddy ameibwa jana (juzi) usiku,” alieleza Nandoo.

Eunice Shaibu (11), alisema: “Aliniita akaniuliza kwa Teddy wapi?” nikamwambia subiri nikuitie mwenzangu akupeleke mimi nimeachwa nilinde nyumba, nikamuita Therezia ndiye aliyempeleka.”

Terezia Michael (11), alisema alipofika nyumbani kwa Teddy, walimkuta akiwa amekaa kwenye kizingiti cha mlango wa kuingia kwenye ua wa nyumba yao akampokea mkoba.

Rosemary Ndahani (21), anayeishi chumba kilichopakana na Teddy, alisema akiwa na mpangaji mwenzao, Happy, waliona Teddy akiingia kwenye ua wa nyumba yao na dada anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 28, mrefu, mweupe mwenye unene wa wastani, alivaa dera ambalo mtandio wake aliutumia kujifunga ushungi.

Alisema hawakufahamu kilichoendelea mpaka asubuhi aliposikia Teddy na mdogo wake wakipiga kelele za kuomba msaada, kufunguliwa mlango wa chumba chao uliokuwa umefungwa kwa nje na kwamba alipotoka chumbani humo alikuwa akiweweseka mithili ya watumiaji wa dawa za kulevya.

“Alichokuwa akitamka ni kudai mtoto wake, akisema ‘wameniibia mtoto wangu, lakini alikuwa hajiwezi, akiweweseka kwa kukosa nguvu kabisa mpaka wazazi wake walipofika na kumpeleka hospitali,” alieleza Ndahani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime, alipoulizwa na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na tukio hilo, alisema analifanyia kazi na kwamba hawezi kuthibitisha kama mtoto huyo ameibwa ama la.
via>>Nipashe

MWANASIASA AAHIDI KULA TAI NA SAA YAKE,MGOMBEA AKISHINDA URAIS,KWELI YATOKEA


Ni bora kuwa mwangalifu hasa kuhusu kile unachoahidi watu maana yanaweza ya kukuta kama yaliyomkuta mwanasiasa mmoja nchini Bolivia.
Mwanasiasa huyu Jorge "Tuto" Quiroga, alikuwa mgombea wa urais katika uchaguzi uliokamilika Jumapili iliyopita nchini Bolivia.
Rais huyo wa zamani ambaye pia alikuwa mpinzani mkuu wa Rais Evo Morales alitoa ahadi moja ambayo ikiwa angejua matokeo kabla ya uchaguzi basi asingedhubutu kuitoa.
Ilikua ahadi ambayo haikuwa na busara.
Aliahidi kula saa yake ikiwa kila wabolivia 'sita' kati ya 'kumi' wangempigia kura Rais Morales.
Jorge "Tuto" Quiroga aliahidi kula saa yake na tai ikiwa Morales angepigiwa kura kwa wingi
Alikuwa na uhakika sana kuwa Morales asingeweza kushinda uchaguzi kiasi cha kutoa ahadi nyingine ya kutatanisha ya kula tai yake katika mahojiano mengine siku chache zilizofuata.
Na sasa mitandao ya kijamii nchini Bolivia Facebook na Twitter imejaa taarifa za wananchi kumtaka mwanasiasa huyo atimize ahadi zake.
 Mwanzo ale saa yake na kisha afuatie ne tai yake.
''Je ni lini ambapo Tuto Quiroga atakula saa yake?'' alihoji mtu mmoja.
Tuffi ArĂ©, mtumiaji maarufu wa Twitter alimhoji bwana Quiroga kabla ya uchaguzi mkuu. 
Yeye alituma ujumbe kwa Twitter akisema labda bwana huyo anasubiri matokeo kamili ya uchaguzi ndipo ale saa yake.
Pia alihidi atakula Tai yake na yote hayo yalinakiliwa.
Ingawa watu wengi nchini Bolivia wametoa maoni yao kwenye Twitter na Facebook, wengi wanaomshinikiza mwanasiasa huyo ni wafuasi wa Rais Evo Morales aliyeibuka mshindi wa uchaguzi huo.
via>>BBC

MSHANGAO MISS TANZANIA 2014, VIGEZO VILIVYOMPA USHINDI MMMMMMHHHHH....


Siku chache baada ya kutwaa Taji la Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu ameibua mshangao wa aina yake kutokana na utata wa umri wake, Ijumaa limesheheni data.
Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu akionesha cheti mara baada ya kuhitimu masomo.
Utata huo uliibuka saa chache mara baada ya shindano hilo kufanyika Oktoba 10, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar ambapo wadau mbalimbali walianza kuhoji.
UTATA WENYEWE HUU HAPA
Mara baada ya mrembo kutangazwa mshindi, habari za chini kwa chini zilidai kwamba Sitti alijinasibu kuwa ana umri wa miaka 18 na elimu ya (digrii mbili) (masters), mambo ambayo yaliwashtua wengi na kuanza kuhoji uhalali wa umri huo ukilinganisha na kiwango chake cha elimu.
“Mh! Haiwezekani, kama ana miaka kumi na nane atakuwa alianza darasa la kwanza akiwa na miaka miwili?” Alihoji mdau mmoja ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini.


ELIMU YA BONGO IKOJE?
Kwa mfumo wa elimu nchini ulivyo, mtoto huanza darasa la kwanza akiwa na kati ya miaka mitano hadi saba, jambo ambalo haliingii akilini kwa Sitti kwani hesabu zinakataa hata kwa mtu asiyesomea mahesabu.

Ukiachilia mbali shule ya awali (nursery) ambayo huchukua kati ya miaka miwili hadi mitatu, ukihesabu miaka saba ya elimu ya msingi (primary), miaka minne ya sekondari (ordinary level), miaka miwili ya kidato cha tano na sita (advanced level) na miaka mitatu ya shahada kwanza (bachelor degree), jumla ni miaka 16.
Mlimbwende, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu.
Pia kuna madai kwamba ametumia mwaka mmoja kusomea shahada ya pili (masters) huku kukiwa na muda ambao kwa kawaida huwa unapotea baada ya kumaliza kidato cha nne kwenda cha tano na baada ya kumaliza kidato cha sita kwenda chuo kikuu.
INA MAANA ALIANZA DARASA LA KWANZA AKIWA NA MIAKA MIWILI?
Kwa mantiki hiyo, kama kweli Sitti ana umri wa miaka 18, basi atakuwa alianza darasa la kwanza akiwa na miaka miwili, jambo ambalo ni msamiati mpya kwa jamii ya Kibongo.
Mrembo, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu akifurahia jambo na marafiki zake wa mamtoni.
BABA MZAZI ANASEMAJE?
Ili kuondoa utata na tafrani inayoendelea kwenye mitandao ya kijamii hadi kufikia hatua ya watu kutukanana, gazeti hili lilimtafuta baba mzazi wa Sitti ambaye ni Mbunge wa Temeke, Dar kwa leseni ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Abbas Zuberi Mtemvu alipopatikana alifunguka:

“Umri wake ni kama alivyosema mwenyewe siku ile (miaka 18), kama mnataka kujiridhisha nendeni hata huko Miss Tanzania mtaoneshwa passport (hati ya kusafiria) yake…,” alisema mzazi huyo huku akiomba aachwe kwanza ashughulikie wananchi wa jimboni kwake.
Sitti Abbas Zuberi Mtemvu akiwa na baba yake, Mhe. Abbas Zuberi Mtemvu.
TUMUAMINI MZAZI?
Hata kama tukiamini maelezo ya mzazi, maana yake ni kwamba mrembo huyo alianza darasa la kwanza akiwa na miaka miwili, jambo ambalo linazidi kuongeza utata katika sakata hilo.

AKATAA KUHITIMU MASTERS
Alipobanwa zaidi kuhusu taarifa zinazosema kuwa mwanaye amehitimu masters, mzazi huyo alikanusha na kudai kwamba mwanaye amehitimu bachelor degree (shahada).
“Kuhusu masters mnakosea, mwanangu hana masters, ana bachelor, nilimshauri achukue masters lakini akaomba nimuache ashiriki kwanza mashindano ya u-miss ndiyo aje aendelee baadaye,” alisema mheshimiwa huyo.
Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu wakati wa kutwaa taji
NI AIBU NYINGINE KWA LUNDENGA?
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, suala la warembo kudanganya umri limekuwa ni sugu hivyo kuleta tafsiri ya aibu kwa muandaaji wa mshindano hayo, Hashim Lundenga akidaiwa kupigwa changa la macho pindi anapowapokea katika mchakato wa awali.
Pasipoti ya kusafiria ya Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu.
“Hii ni aibu nyingine kwa Lundenga kwani haiwezekani mtu akaingia akasema ana miaka kumi na nane halafu awe na elimu kama hiyo, anashindwaje kulibaini hilo mapema?” Alihoji mdau mkubwa wa urembo nchini akikumbushia kisa cha Wema Isaac Sepetu, Miss Tanzania 2006/07 ambaye naye alidanganya umri akasema ana miaka 18 wakati alikuwa na kumi na saba.
Leseni ya udereva ya Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu.
MSIKIE LUNDENGA SASA
Alipotafutwa Lundenga ili kuzungumzia suala hilo, alijibu kwa kifupi na kukata simu:
“I can’t answer that question (Siwezi kujibu swali hilo)…siwezi.”

SITTI ANASTAHILI KUWA NA UMRI GANI?
Ukiachilia mbali muonekano, baadhi ya watu waliozungumza na gazeti hili walisema kuwa ukifuata utaratibu wa mfumo wa elimu Bongo, Sitti alipaswa angalau awe na umri wa miaka 23, hata kama madai ya kurushwa madarasa ni sahihi.

Muandaaji wa mshindano ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga akifafanua jambo
Yaani angeanza darasa la kwanza akiwa na miaka saba, angesoma shule ya msingi kwa miaka saba, sekondari miaka minne, kidato cha tano na sita miaka miwili na chuo miaka mitatu, jumla angekuwa na umri wa miaka 23 kwa sasa ambayo ni pungufu ya miaka 25 iliyotajwa kwenye wasifu wake mtandaoni huko nchini Marekani. 

SITTI AMEFIKAJE HAPA?
Data zinaonesha kwamba, baada ya kumaliza kidato cha sita, Sitti alihamia jijini Dalas kwenye Jimbo la Texas, Marekani ambapo mbali na kusomea elimu ya chuo kikuu nchini humo, amewahi kuigiza filamu inayojulikana kwa jina la Lost In Abroad.


CHANZO, GAZETI LA IJUMAA

MCHUNGAJI ATOROSHA MKE WA MTU


Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa kasi, Janet Mrema anayedaiwa kutoroshwa na mchungaji huyo.
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa kasi, Janet Mrema anayedaiwa kutoroshwa na mchungaji huyo.
Mchungaji anayejiita nabii na mtume, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) aliyetajwa kwa jina moja la Emmanuel amejikuta ndani ya majanga kufuatia madai mazito kwamba amemtorosha mke wa mtu ambaye ni mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa kasi, Janet Mrema.
Kwa mujibu wa chanzo makini, mchungaji huyo alifika nyumbani kwa Jonas Mrema, mume wa Janet, maeneo ya Tegeta-Nyaishozi jijini Dar na kuishi kama mtumishi wa Mungu lakini polepole alianza mazoea tata na Janet.
 
“Mume alianza kuhisi mabadiliko ya mkewe kwa mtumishi huyo, lakini nadhani aliona ni mawazo yake tu. Ndipo siku ya siku akashangaa mkewe na mchungaji huyo wameondoka nyumbani hapo.
 
“Kwa sasa tangu tukio hilo litokee ni miezi kama mitatu. Mume alihangaika sana kumtafuta mkewe hadi jana (Jumatatu iliyopita) ndipo akampata wakiwa na mchungaji huyo kwenye nyumba moja ambako walikuwa wakiishi pamoja,” kilisema chanzo chetu.
Iliidaiwa kwamba, mchungaji huyo alipopekuliwa alikutwa na paspoti ya nchini Burundi wakati yeye ni Mkongo wa Uvira na alionekana kuishi nchini kinyume na sheria hivyo alifunguliwa jalada la kesi kwenye Kituo cha Polisi cha Wazo Hili, Tegeta lenye Kumbukumbu Na. WH/RB/7040/2014- KUISHI NCHINI BILA KIBALI.
 

Juzi, Amani liliwasiliana na Katibu wa Chama cha Waimba Injili Tanzania, Stela Joel ambaye alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema tayari chama hicho kimemsimamisha uanachana Janet kwa kitendo chake hicho cha kumtoroka mumewe wa ndoa.
 
“Ni kweli na Chama cha Waimba Injili Tanzania kimemsimamisha uanachama Janet. Hatuna mzaha katika maadili,” alisema Stela.
 
Amani lilimpigia simu mume wa Janet, Jonas Mrema ambapo katika mazungumzo baada ya salamu alipewa pole kwa matatizo ya mkewe, alisema asante kisha alipoulizwa kuhusu hali ilivyo aliomba apige simu yeye baadaye kwa vile alikuwa kikaoni.
 
Hata hivyo, baada ya saa mbili kupita bila kupiga, Amani lilimpigia tena simu ambapo iliita bila kupokelewa hivyo jitihada za kumpata zinaendelea.