Kwenye kikao cha Bunge November 20 2014 Dodoma Hatibu ambae ni mbunge wa Zanzibar aliuliza >>> “…
Sisi wabunge wa bunge hili ndiyo wapiga kura wa kuwachagua wawakilishi
wetu wa kutuwakilisha katika bunge la Afrika Mashariki, kumekuwa na
taarifa za kulipaka Taifa hili matope kulitia aibu kutokana na baadhi
ya wawakilishi wetu, Wabunge wetu wa Afrika Mashariki kutokana na
matendo wanayoyafanya kule..”
“…Ni
lini hasa kinachoendelea pale na hatua gani zilizochukuliwa kuhusu
ukosefu wa nidhamu uliojitokeza kwa mbunge Shyrose Banji wazi wazi na
bili hali hakuna taarifa yoyote, Mheshimiwa Naibu Spika naomba mwongozo
wako…”– Hatibu.
Baada ya swali waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akawasha kipaza sauti na kutoa haya majibu “…Naomba
nitoe taarifa kwamba kinachotokea katika Bunge la Afrika Mashariki kwa
kiasi kikubwa kinahusu mgogoro wa spika mwenyewe, hilo ndiyo chanzo cha
matatizo mengi, kwa hiyo wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki
wamegawika kataka makundi mawili, kuna kundi linalotaka Spika lazma
aondolewe, na wengine wanadai wanamtetea abaki…”
“…Katika
tukio ambalo limetokea juzi na nasema hivi kwa sababu Naibu Waziri
wangu yuko kule kwa hiyo ni jambo halisi, kilichotokea sio kama
kinavyoelezwa Mheshimiwa Shyrose Banji ambaye anahesabika ni mfuasi
mkubwa wa Yule Spika kiasi kwamba wenzie wanamuona kama kibaraka vile,
alikuwa anapita katikati ya Wabunge wengine kuwahi usafiri kwa bahati
mbaya akamgonga Mheshimiwa Ndelakindo Kessy, Mheshimiwa Ndelakindo
akahamaki na kwa kusaidiwa na baadhi ya Wabunge wengine wa Uganda
akaenda kituo cha Polisi kutoa taarifa kwa madai kwamba amefanyiwa
makosa ya jinai wanaita ‘assaults’…“– Sitta.
“
“>…Ikabidi aitwe ‘Sergeant at Arms’ wa Bunge la EALA ambaye
alikwishaanza jitihada za kulifanya jambo lile liishie ndani ya Bunge na
katika jitihada hizo alifika mbali kidogo akawezesha Wabunge wetu hao
wawili waweze kusikilizana na ninavyotoa taarifa hivi sasa ni kwamba
jana suala hili limekwisha na haliendelezwi na Polisi tena…
“– Sitta.
Hivi ndivyo Waziri Sitta alimalizia kujibu suala hilo; “…Sasa
yale mengine yaliyosema kwamba alifanya mambo ya hovyo Mheshimiwa yule
tena kama miezi miwili iliyopita, bado yako mikononi mwa tume ya Bunge
la Afrika Mashariki hadi hapo watakapolishughulikia hatuwezi kufanya
kitu chochote, na tukishapata taarifa ya tume ya Bunge la Afrika
Mashariki basi mimi nitatoa taarifa kwa Mheshimiwa Spika ili sasa sisi
kwa wote kama jimbo la uchaguzi La Wabunge hao tuone ukweli ni upi na
tujue hatua ya kuchukua..”– Sitta.
Kama ukihitaji kusikiliza maswali na majibu hayo kutoka kwenye kikao cha bunge, bonyeza play hapa.
Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio
Related Posts
- HATIMAYE KINACHOWAUA WASANII KWA KASI CHAJULIKANA!! SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI..25 Dec 20140
MWAKA 2014 unakatika, matukio ya kukumbukwa ni pamoja na wasanii Bongo kupoteza maisha katika maz...SOMA ZAIDI»
- PICHAZ: MTUMZIMA SUPER STAR SINGER PATCHO MWAMBA ALA KIPIGO CHA MBWA MWIZI KWA KUBAMBWA NA MKE WA MTU!!25 Dec 20140
Picha kwa hisani ya @selfielife instagram Inasemekana kuwa mwigizaji na mwanamuziki wa Dan...SOMA ZAIDI»
- TABIA ZA MSICHANA ANAYEPENDA LAKINI HAWEZI KUSEMA NI HIZI HAPA.23 Dec 20140
1. Atakutega kupata attention yako. Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda au l...SOMA ZAIDI»
- NJIA YA KUPATA MTOTO WAKIKE AMA WAKIUME NI HII HAPA23 Dec 20140
Ni vipi jinsia ya mtoto huainishwa?Kinyume na wengi wanavyofikiria kwamba mwanamke au mwil...SOMA ZAIDI»
- WATOTO WA KIKE NA MAPENZI YA HARAKA HARAKA- WAKINA MAMA JE MNAWAELIMISHAJE NA KUWAKUZA WATOTO WA KIKE ILI KUWAANDAA KUPAMBANA NA MAISHA YA KIMAPENZI?23 Dec 20140
Hivi ni mimi tuu bado niku nyuma ama ndo kuamka kwa tamaduni zetu za kiafrika? Siku hiz...SOMA ZAIDI»
- MWALIMU ANYONGA MTOTO GESTI,MWILI WAHIFADHIWA KWENYE KORIDO HOSPITALI HAINA MOCHWARI21 Dec 20140
Askari wa jeshi la polisi wakiwa eneo la hospitali ya wilaya ya Mbogwe mkoani Geita Mwili w...SOMA ZAIDI»
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.