“…Naomba
mwongozo wako kwamba kinachoendelea katika viwanja hivi vya Bunge pale
Kantini, kuna mabadiliko makubwa sana yamefanyika kwa watoa huduma
kiasi kwamba kwanza hata huduma zao na kauli zao kwa wateja wao sisi
wabunge sio nzuri..“, Hiyo ilikuwa kauli ya mwongozo wa Mbunge
Martha Mlacha alipopewa nafasi kutoa mwongozo wake katika kikao cha
Bunge leo Dodoma.
“…Lakini
kitu ambacho.. ninachokuomba mwongozo kwamba Bunge hili.. hapa mahali
hapa.. ndiyo chimbuko na kisima cha watetea haki za Watanzania wote,
wakiwemo vibarua, wafanyakazi na watu wengine na kwamba kama kuna
kampuni inachukua ama kufanya biashara kwenye eneo fulani ikakuta
wafanyakazi maeneo yale, inabidi wafanyakazi wa eneo lile wachukuliwe na
kampuni ile inayokuja pale…”– Mlata.
“…Kumetokea
sintofahamu naomba mwongozo wako, hivi sasa vijana thelathini waliokuwa
wanafanya kazi katika kwenye kantini ile wanarandaranda mitaani
wanakutana na sisi wabunge wakituomba tuwasaidie hata hela ya kula,
naomba mwongozo wako ni nini kimetokea?..”– Mlata.
Akijibu mwongozo huo Naibu Spika; “…
Hili ambalo ameliongea Mheshimiwa Mlatha ni jambo la ndani.. ni jambo
la kwetu sisi wenyewe, niwahakikishieni waheshimiwa Wabunge kwa kifupi
sana kwamba jambo hili liko mikono salama ya tume ya huduma za Bunge,
mabadiliko hayo ni kwa nia njema watumishi waliokuwa pale wengi wao
wamekuwa deployed tayari maeneo mengine ya kazi..“– Ndugai.
“…Nawapa
majibu ya uhakika, zaidi ya robo tatu wameshakuwa deployed tayari na
tulikuwa na kamati ya tume jana wala sio juzi na tumelizungumzia jambo
hili , wako vijana wachache ambao bado hawajachukuliwa, na hao wachache
watachukuliwa watapangwa katika maeneo mengine ya shughuli. Kwa hiyo
liko mikono salama kabisa…“– Ndugai.
Nimekuwekea sauti ya Mbunge huyo na Naibu Spika wakati ukitolewa mwongozo huo, unaweza kusikiliza kwa kubonyeza play hapa.
Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio
Related Posts
- HATIMAYE KINACHOWAUA WASANII KWA KASI CHAJULIKANA!! SOMA HAPA KWA HABARI KAMILI..25 Dec 20140
MWAKA 2014 unakatika, matukio ya kukumbukwa ni pamoja na wasanii Bongo kupoteza maisha katika maz...SOMA ZAIDI»
- PICHAZ: MTUMZIMA SUPER STAR SINGER PATCHO MWAMBA ALA KIPIGO CHA MBWA MWIZI KWA KUBAMBWA NA MKE WA MTU!!25 Dec 20140
Picha kwa hisani ya @selfielife instagram Inasemekana kuwa mwigizaji na mwanamuziki wa Dan...SOMA ZAIDI»
- TABIA ZA MSICHANA ANAYEPENDA LAKINI HAWEZI KUSEMA NI HIZI HAPA.23 Dec 20140
1. Atakutega kupata attention yako. Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda au l...SOMA ZAIDI»
- NJIA YA KUPATA MTOTO WAKIKE AMA WAKIUME NI HII HAPA23 Dec 20140
Ni vipi jinsia ya mtoto huainishwa?Kinyume na wengi wanavyofikiria kwamba mwanamke au mwil...SOMA ZAIDI»
- WATOTO WA KIKE NA MAPENZI YA HARAKA HARAKA- WAKINA MAMA JE MNAWAELIMISHAJE NA KUWAKUZA WATOTO WA KIKE ILI KUWAANDAA KUPAMBANA NA MAISHA YA KIMAPENZI?23 Dec 20140
Hivi ni mimi tuu bado niku nyuma ama ndo kuamka kwa tamaduni zetu za kiafrika? Siku hiz...SOMA ZAIDI»
- MWALIMU ANYONGA MTOTO GESTI,MWILI WAHIFADHIWA KWENYE KORIDO HOSPITALI HAINA MOCHWARI21 Dec 20140
Askari wa jeshi la polisi wakiwa eneo la hospitali ya wilaya ya Mbogwe mkoani Geita Mwili w...SOMA ZAIDI»
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.