Stori: Mayasa Mariwata
STAA wa filamu Bongo ambaye miezi michache iliyopita alifunga pingu za maisha na mwanaume mwenye asili ya Denmark, Lucy Komba amekwea pipa kuelekea nchini humo kwenda kuishi na mumewe sambamba na kumpelekea mwanaye amlee.
Staa wa filamu Bongo, Lucy Komba akiwa na mume wake(mdenmark) wakati wa harusi yao.
Akipiga stori na paparazi wetu kupitia Mtandao wa WhatsApp akiwa nchini Denmark, Lucy alisema aliamua kuondoka kimyakimya na kumfuata mumewe kwa kuwa alimisi mambo mengi kwake, pia suala la ndoa halimuhitaji aishi mbali na mumewe na kwa kuwa mwanaume huyo anampenda sana mtoto wake japo hajazaa naye ndiyo maana akaamua kuondoka naye akamlee.
“Najua mtu anaweza kuongea vyovyote, mimi nilimmisi mume wangu na mwanangu naye alitamani sana kuja kumsalimia baba yake ndiyo maana nikamleta huku amlee ila baadaye atarejea Bongo,” alisema Lucy.

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top