. Kocha Juma Mwambusi ameuandikia barua uongozi wa Mbeya City ya kubwaga manyanga kuinoa timu hiyo kwa kuchoshwa na kelele za shutuma dhidi yake.
Mbeya City imeanza vibaya Ligi Kuu Bara msimu huu kwani inashika mkia ikiwa na pointi tano baada ya kucheza michezo saba, imeshinda mmoja, imetoa sare miwili na kufungwa minne.
Kufanya vibaya kwa timu hiyo kumeibua maneno mengi hasa wakimtuhumu Mwambusi kuwa ameshindwa kazi na ndio sababu uwez wa timu hiyo umeporomoka.
Kutokana na jambo hilo, kocha huyo wa zamani wa Prisons ameamua kuachia ngazi ili kuwapisha wengine baada ya kuchoshwa na maneno mengi yanayoelekezwa kwake.
Mwamabusi aliliambia gazeti hili jana kuwa ameamua kujiweka pembeni ili kuwapisha makocha wengine watakaoweza kuinoa timu hiyo na kuipa mafanikio.
“Maneno ni mengi sana baada ya matokeo haya na wengi wanaelekeza maneno haya kwangu kuwa sifai, mimi mkali, hivyo nimeona bora niwaachie timu yao ili kulinda heshima yangu.“Nimekaa na timu hii kwa miaka minne, nimeipandisha daraja, nimekaa na wachezaji wangu vizuri na msimu uliopita tukafanya vizuri lakini msimu huu mambo yamekuwa tofauti na maneno mengi yameongelewa, mengine yamehusisha familia yangu,” alisema na kuongeza: “Leo naaambiwa eti mimi mkali ndio sababu wachezaji wanashindwa kucheza kwa kiwango, lakini miaka yote nimekaa na timu mbona sikuambiwa hivyo. Alipoulizwa katibu wa klabu hiyo, Emmanuel Kimbe kama wamepokea barua ya kocha huyo, alisema hadi wakati huo hakukuwa na barua ya Mwambusi.
 
   

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top