pinguWaandishi wa habari watatu walioshtakiwa kwa kuandika habari za kichochezi huenda wakaachiwa huru hivi karibuni kwa msamaha wa Rais.
Waandishi wa Habari hao Peter Greste raia wa Australia, Mohammed Fahmy mwenye asili ya Canada na Baher Mohammed wanashikiliwa Misri ambako walihukumiwa kifungo baada ya kukutwa na hatia ya kukisaidia chama cha Muslim Brotherhood na kueneza habari za kupendelea upande wa Kikundi hicho.
Mohammed Fahmy, Peter Greste, Baher Mohamed
Rais wa Misri, Abdi Fatah El Sisi amesema msamaha huo utatolewa kama hakutakuwa na athari yoyote kwa nchi hiyo kiusalama.
Waandishi wawili kati yao walihukumiwa kifungo cha miaka 10, mmoja wao akihukumiwa kifungo cha miaka 7.

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top