MISS Sinza 2001 na aliyekuwa mshiriki wa Miss Tanzania 2011, Husna Maulid.
Na Gladness Mallya
HAMNAZO? MISS Sinza 2001 na aliyekuwa mshiriki wa Miss Tanzania 2011, Husna Maulid ameonesha kuwa ni sikio la kufa baada ya kupiga picha za utupu kwa mara nyingine.
Picha hizo zilizotapakaa kwenye mitandao mbalimbali zimewashangaza watu ambapo Husna anaonekana akiwa kama alivyozaliwa huku akiwa katika mapozi tofauti hali inayoonesha kwamba alikuwa akipigwa picha hizo na mpenzi wake.
Husna Maulid akiwa kwenye pozi lenye utauta!.
Kwa mujibu wa mdau ambaye aliziweka picha hizo kwenye mtandao wa Instagram, mwanadada huyo alipigwa picha hizo na mpenzi wake ambaye hakumtaja jina.Alisema mpenzi wake huyo alimuomba ampige picha ili awe anaziangalia kila wakati kwani anampenda sana ambapo Husna alikubali kupigwa picha hizo lakini matokeo yake zikazagaa mitandaoni.


Watu mbalimbali waonesha kushangazwa na picha hizo huku wengine wakimkashfu kwa maneno machafu.
Baada ya kuzinyaka picha hizo, Amani lilimtafuta Husna na kumuuliza ilikuwaje mpaka akakubali kupiga picha hizo za ajabu, alisikiliza kwa makini kisha akakata simu na alipotafutwa tena simu yake ilikuwa ikiita tu bila kupokelewa.

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top