Manchester-UnitedClub hii imeripotiwa kumsajili kipa wa zamani wa Barcelona na timu ya taifa ya Hispania Victor Valdez baada ya kufanya nae mazoezi kwa muda wa karibu mwezi mzima.
Valdez ambaye aliihama Barcelona baada ya mkataba wake kuisha msimu uliopita alikuwa karibu kujiunga na Liverpool lakini jeraha baya la goti alilopata katikati ya msimu uliopita  lilizuia usajili wake kwenda Anfield.
Victor Valdez yuko mbioni kukamilisha usajili wake na Manchester United .
Victor Valdez yuko mbioni kukamilisha usajili wake na Manchester United .
Katika kipindi hiki kocha wa Manchester United Louis Van Gaal alimpa kipa huyo nafasi ya kufanya mazoezi na United hali ambayo ilimuweka karibu na usajili ndani ya klabu hiyo .
Usajili wa Valdez ulithibitishwa na kipa namba moja wa United David De Gea ambaye alizungumza na waandishi wa habari na kuwathibitishia kuwa United imemsajili Valdez.
De Gea aliwaambia waandishi kuwa United haijamsajili Valdez kama mbadala wake.
De Gea aliwaambia waandishi kuwa United haijamsajili Valdez kama mbadala wake.

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top