Jana jioni nilipotoka kazini nikapitiliza nyumbani, nipo na mchumba wangu kama mwezi hapa alikuja kunitembelea. 

Nilipofika nikamkuta anaangalia tamthilia, nikavua nguo nikaenda kuoga.


Ukweli njaa ilikuwa imenibana kishenzi.

Nilivyotoka bafuni nikaambiwa, baby leo zamu yako kupika, nikadhani nimesikia vibaya, nikamuuliza tena na kupewa jibu lile lile. 

Nikavaa nguo nikaenda zangu pub nikaagiza chakula nikala(sio kwamba kupika siwezi ila kupangiwa ratiba).
Nilivyorudi nyumbani nikapitiliza moja kwa moja kulala. 

Baada ya muda akaanza kunifokea na kuniambia nilikuwa kwa malaya wangu na nimekula huko.

Nilipatwa na hasira nikamtandika vibao. Asubuhi tumeamka ananiambia anataka kuondoka, nikampa nauli na kumtakia safari njema. 

Nikamwambia ‘umepoteza maksi zaidi ya nusu'.
Mpaka sasa hajaondoka na anaomba tuyamalize.

Wadada, hata kama umesoma kiasi gani mambo ya haki sawa na kupangiana ratiba hayapo dunia hii. Nitapika siku nikijisikia na sio uanze kunipangia ratiba ya kupika.

Ugomvi mwingine mnautafuta bila sababu za msingi. 

Bora hata angeniambia naomba tusaidiane kupika leo

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top