Stori: Gladness Mallya
MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amefunguka kuwa japokuwa ana watoto wengine wa nje lakini anajivunia kuzaa na mkewe, Siwema kwani walipitia changamoto nyingi kabla ya kupata mtoto.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ akiwa na mpenzi wake Siwema.
Akichezesha taya na paparazi wetu, Nay alisema katika maisha ya mapenzi yake na Siwema walivumilia vingi na hivi sasa ana mshukuru Mungu kwani wameweza kufikia hatua nzuri ya kupata mtoto.

“Maisha ya mapenzi yetu yalikuwa na changamoto sana lakini nilisimama kwa sababu nampenda mke wangu Siwema, najivunia kuzaa na Siwema mtoto wa kiume na ninaendelea kumuomba Mungu aendelee kumkuza mwanetu,” alisema Nay wa Mitego.

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego

Wadau mbalimbali wamekuwa wakimpongeza Nay kwenye mitandao ya kijamii kwa kile wanachodai kwamba ana mapenzi ya kweli licha ya changamoto nyingi zilizojitokeza kwa mpenzi wake Siwema za picha kuzagaa mitandaoni kwamba alikuwa mchumba wa mtu.

Soma Nafasi za kazi na ajira bofya hapa chini kutizama, Mjulishe na mwenzio

Facebook Blogger Plugin by Bongo na Matukio

Post a Comment

 
Top